Wafungwa Kifungo cha Maisha Jela Kwa Kumbaka Mama Mbele ya Mumewe na Watoto - OREST NGOWI

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Tuesday, 2 August 2016

Wafungwa Kifungo cha Maisha Jela Kwa Kumbaka Mama Mbele ya Mumewe na Watoto

   
Mwendesha mashitaka huyo alisema wanafamilia hao kupitia mwanga wa taa ya sola waliweza kuwatambua watuhumiwa kabla wazazi hawajapelekwa Hospitali ya Misheni Chimala walikolazwa kwa ajili ya matibabu.


Kutokana na makosa hayo Luchagula aliiomba Mahakama kutoa adhabu kali kwa washitakiwa ili iwe fundisho kwa watu wengine walio na tabia hizo wilayani hapa na kwingineko nchini.

Akito adhabu kwa washitakiwa, Hakimu Mkasela alisema ameridhishwa na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo na pande zote mbili na kwamba kwa kosa la kwanza la unyangaji wa kutumia silaha washitakiwa watakapaswa kutumikia kifungo cha miaka 30 jela na kwa kosa la pili la ubakaji watatumikia kifungo cha maisha jela ili iwe fundisho kwao na watu wengine.


Awali washitakiwa waliiomba Mahakama kuwapunguzia adhabu wakisema bado umri wao ni mdogo na wanategemewa na familia zao, maombi ambayo yalitupiliwa mbali na hakimu Mkasela.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here