Mifuko ya ifadhi jamii yaanza kuwekeza kwenye viwanda - OREST NGOWI

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Monday, 5 September 2016

Mifuko ya ifadhi jamii yaanza kuwekeza kwenye viwanda

   Image result for picha jenista mhagama
Serikali imesema imejipanga kuishirikisha mifuko ya jamii kikamilifu katika kuhakikisha mchango wake unatumika kikamilifu kuleta maendeleo na uchumi wa viwanda.

Kauli hiyo imetolewa mkoani Dodoma na waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu, sera, bunge, kazi, vijana,ajira na wenye ulemavu, Jenista Muhagama, wakati wa mkutano ulioshirikisha watengaji wa wizara nne.
“Juzi NSSF wamekabidhi cheki ya bilioni kama mbili pointi moja tayari kwa utekelezaji wa ujenzi wa viwanda katika nchi yetu ya Tanzania, kiwanda cha kuua vijidudu na hasa viluwiluwi vinavyozalisha Malaria pale kibaha,” alisema.
“BC wameshapokea pesa kupitia benki ya Azania, sasa kazi kwako mzee wa viwanda, simama imara pale, kiwanda kile kifanye kazi vizuri,fedha yetu ya mifuko ya wanachama iweze kurejeshwa kwa wakati na kwa faida,” alisema Muhagama.
Pia Muhagama aliongezea kuwa lengo la kuanisha mchango wa mifuko ya hifadhi ya jamii ni kuiwezesha Tanzania kufikia uchumi wa viwanda kufikia mwaka 2025.

BY: EMMY MWAIPOPO

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here