WANAOWAPATIA MIMBA WATOTO WA SHULE KUKIONA CHA MOTO. - OREST NGOWI

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Thursday, 22 September 2016

WANAOWAPATIA MIMBA WATOTO WA SHULE KUKIONA CHA MOTO.

Responsive Ads Here
  _DSC0447
Mkuu wa wilaya ya Geita,Herman Kapufi akizungumza na watendaji katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Geita.
Mkuu wa Wilaya ya Geita,Hermani Kapufi,amewaagiza maafisa watendaji  wa kata,vijiji na vitongoji kushughulika na wale wote ambao watabainika wamewapatia ujauzito wanafunzi ambao bado wapo masomoni.

Kauli hiyo ,ameisema wakati alipokutana na watendaji katika kikao cha pamoja kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri ya Wilaya ya Geita ambacho kilikuwa kimelenga kutatua changamoto za watendaji wa kata,vijiji na vitongoji.
Amesema kuwa suala la baadhi ya watu kuendelea kuwapa mimba watoto wa shule  limekuwa ni changamoto ambayo imesababisha kukatisha ndoto za baadhi ya wanafunzi kwa kuwashawishi kwa vitu vidogo na mwisho wa siku kuwapotezea ndoto zao pamoja na mlengo waliyojiwekea.
“Natambua kuwa kuna tatizo kubwa linaloendelea kwa maeneo ya hapa wilayani kwa watu kuendelea kuwapa mimba wanafunzi na mwisho wa siku hakuna sheria yoyote inayochukuliwa mimi nikiwa kama Mkuu wa wilaya hii ninawaagiza watendaji wote kuwashughulikia wale wote ambao wanatabia ya namna hiyo serikali inawekeza fedha nyingi sana kwa wanafunzi leo hii wanatokea baadhi ya watu kukatisha ndoto zao kamwe hatuwezi kuwafumbia macho watu wenye tabia za namna hiyo”alisema Kapufi.


Aidha kwa upande wao watendaji  wamesema kuwa matatizo ya baadhi ya watu kuwapa mimba wanafunzi yapo mengi sana katika maeneo wanayo yaongoza na kutokana na agizo hilo wanaamini kuwa wataweza kuwaadhibu wale ambao wamekuwa na tabia za namna hiyo.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad